Posts

Showing posts from November, 2022

Cha Kutumaini sina.

Image
  1. Chakutumaini sina Ila damu yake Bwana, Sina wema wa kutosha Dhambi zangu kuziosha;  Kwake Yesu na Simama,  Ndiye mwamba: ni salama  Ndiye mwamba: ni salama. 2. Njia yangu iwe ndefu Yeye hunipa wokovu; Mawimbi yakinipiga Nguvu zake ndiyo nanga. 3. Damu yake na sadaka Nategemea daima, Yote chini yakiisha Mwokozi atanitosha. 4. Nikiitwa hukumuni, Rohoni nina amani Nikivikwa haki yake Sina hofu mbele zake.

Yesu Kwa imani

Image
1. Yesu kwa imani, Nakutumaini, Peke yako; Nisikie sasa, Na kunitakasa, Ni wako kabisa Tangu leo. 2. Nipe nguvu pia Za kusaidia Moyo wangu; Ulikufa wewe, Wokovu nipewe Nakupenda wewe, Bwana wangu. 3. Hapa nazunguka Katika mashaka, Na matata; Palipo na giza Utaniongoza Hivi nitaweza Kufuata. 4. Takuwa mzima Nivushe salama Mautini; Sina hofu kamwe Ukiwapo name Nami nikwandame Siku zote.

Tafuta Daima Utakatifu

Image
1. Tafuta daima utakatifu; Fanya urafiki na Wakristo tu; Nena siku zotena Bwana wako, Baraka uombe kwa kila jambo. 2. Tafuta daima utakatifu; Uwe peke yako ukimwabudu; Ukimwangalia mwokozi wako, Utabadilishwa kama alivyo. 3. Tafuta daima utakatifu; Kiongozi wako aew Yesu tu; Katika furaha au huzuni Dumu kumfuata Yesu Mwokozi. 4. Tafuta daima utakatifu; Umtawaze Roho moyoni mwako; Akikuongoza katika haki, Hufanywa tayari kwa kazi yake.

Ewe Roho Wa Mungu

Image
  1. Ewe Roho wa Mbinguni Uje kwetu sasa. Ufanye makazi yako Ndani ya Kanisa. 2. Ndiwe mwanga, umulike Tupate jikana; Mengi kwetu yapunguka, Tujalize, Bwana. 3. Ndiwe Moto, teketeza Taka zetu zote: Moyo na iwe sadaka Ya Mwokozi, yote. 4. Ndiwe Umande, na kwako Tutaburudika, Nchi kavu itakuwa Ni yenye Baraka. 5. Roho wa Mbinguni uwe Nasi hapa chini, Mwili uufananishe Na kichwa Mbinguni.

Nina Haja Nawe

Image
  1. Nina haja nawe Kila saa; Hawezi mwingine Kunifaa.  Yesu, nakuhitaji  Vivyo kila saa!  Niwezeshe, Mwokozi,  Nakujia. 2. Nina haja nawe;  Kaa nami,  Na maonjo haya,  Hayaumi. 3. Nina haja nawe;  Kila hali,  Maisha ni bure,  Uli mbali. 4. Nina haja nawe,  Nifundishe  Na ahadi zako  Zifikishe. 5. Nina haja nawe,  Mweza yote,  Ni wako kabisa  Siku zote.

Usinipite Mwokozi

Image
  1. Usinipite Mwokozi, Unisikie; Unapozuru wengine, Usinipite.  Yesu,Yesu,  Unisikie;  Unapozuru wengine,  Usinipite. 2. Kiti chako cha rehema, Nakitazama; Magoti napiga pale, Nisamehewe. 3. Sina ya kutegemea, Ila Wewe tu; Uso wako uwe kwangu; Nakuabudu. 4. U Mfariji peke yako; Sina Mbinguni, Wala duniani pote, Bwana mwingine

Yesu Kwetu ni Rafiki

Image
  1. Yesu kwetu ni rafiki, Hwamiwa haja pia; Tukiomba kwa Babaye Maombi asikia; Lakini twajikosesha, Twajitweka vibaya; Kwamba tulimwomba Mungu Dua angesikia. 2. Una dhiki na maonjo? Una mashaka pia. Haifai kufa moyo, Dua atasikia Hakuna mwingine mwema Wa kutuhurumia; Atujua tu dhaifu; Maombi asikia. 3. Je, hunayo hata nguvu, Huwezi kuendelea, Ujapodharauliwa Ujaporushwa pia, Watu wange kudharau, Wapendao dunia, Hukwambata mikononi, Dua atasikia.

Taji Mvikeni

Image
  1. Ni tabibu wa karibu; Tabibu wa ajabu; Na rehema za daima; Ni dawa yake njema.  Imbeni, malaika,  Sifa za Yesu Bwana;  Pweke limetukuka  Jina lake Yesu. 2. Hatufai kuwa hai, Wala hatutumai, Ila kweli yeye ndiye Atupumzishaye. 3. Dhambi pia na hatia Ametuchukulia; Twendeni na amani Hata kwake Mbinguni. 4. Huliona tamu jina La Yesu Kristo Bwana, Yuna sifa mwenye kufa Asishindwe na kufa. 5. Kila mume asimame, Sifa zake zivume; Wanawake na washike Kusifu jina lake. 6. Na vijana wote tena, Wapendao sana Waje kwake wawe wake Kwa utumishi wake.

Ni Tabibu Wa Karibu

Image
  1. Taji mvikeni, Taji nyingi tena, Kondoo mwake kitini, Bwana wa mabwana; Name tamsifu Alikufa kwangu, Ni mfalme mtukufu, Mkuu wa Mbingu. 2. Taji mvikeni Mwana wa bikira; Anazovaa kichwani Aliteka nyara; Shiloh wa wanabii, Mchunga wa watu, Shina na tanzu vya Yese, Wa Bethirehemu. 3. Taji mvikeni Bwana wa mapenzi; Jeraha zake ni shani Ni vito vya enzi, Mbinguni hakuna Hata malaika Awezaye kuziona Pasipo kushangaa.

Baba Mwana Roho

Image
  1. Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi, Kila tukiamka tunakuabudu Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi, Ewe Utatu, tunakusifu. 2. Baba, Mwana, Roho, wakuaminio Wanakutolea shukrani zao Wanakusujudia malaika nao: Wewe u mwanzo, nawe u mwisho. 3. Baba, Mwana, Roho, sisi tu gizani, Utukufu wako hatuoni kosa; U Mtakatifu, nawe u mapenzi, U peke yako, mwenzio huna. 4. Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi, Ulivyoviumba vyote vyakusifu: Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi Ewe Utatu, tunakusifu.

Jina Lake Yesu Tamu

Image
  1. Jina lake Yesu tamu; Tukilisikia Hutupoza, tena hamu Hutuondolea. 2. Roho iliyoumia Kwalo hutibika, Chakula, njaani pia; Raha, tukichoka. 3. Jina hili ni msingi, Ngao, ngome, mwamba, Kwa hili napata wingi, Kwangu ni akiba. 4. Yesu, Mchunga, Rafiki Mwalimu, Kuhani, Mwanzo, Mwisho, Njia, Haki, Uzima kifoni. 5. Moyo wangu hauwezi, Kukusifu kweli, Ila sifa zangu hizi, Bwana zikubali. 6. Na utakaponiita, Kuja kwako Bwana, Huko kwako sitaacha Kukusifu sana.

Jina La Yesu Salamu.

Image
  1. Jina la Yesu, Salamu! Lisujudieni, Ninyi Mbinguni, hukumu Na enzi mpeni. 2. Enzi na apewe kwetu, Watetea dini; Mkuzeni Bwana wenu, Na enzi mpeni. 3. Enyi mbegu ya rehema, Nanyi msifuni; Mmeponywa kwa neema, Na enzi mpeni. 4. Wenye dhambi kumbukeni Ya msalabani, Kwa furaha msifuni, Na enzi mpeni. 5. Kila mtu duniani Msujudieni, Kote-kote msifuni, Na enzi mpeni. 6. Sisi na wao pamoja Tu mumo sifani, Milele sifa ni moja, Ni “Enzi mpeni.”

Hata ndimi elfu.

Image
  1. Hata ndimi elfu elfu, Hazitoshi kweli Bwana Yesu kumsifu, Kwa zake fadhili. 2. Yesu, jina liwezalo Kufukuza hofu; Lanifurahisha hilo, Lanipa wokovu. 3. Jina hilo ni uzima; Ni afya amani; Laleta habari njema; Twalipiwa deni. 4. Yesu huvunja mapingu Ya dhambi moyoni; Msamaha, tena nguvu, Twapata rohoni. 5. Kwa sauti yake vile Wafu hufufuka Wakafurahi milele, Pasipo mashaka. 6. Ewe Yesu wangu Bwana, Uwezo nipewe, Kuhubiri kote sana, Wote wakujue.

Twamsifu Mungu

Image
  1. Twamsifu Mungu kwa Mwana wa Pendo, Aliyetufia na kupaa juu.  Aleluya! Usifiwe; Aleluya! Amin.  Aleluya! Usifiwe, utubariki. 2. Twamsifu Mungu kwa Roho Mtukufu, Ametufunulia Mwokozi wetu. 3. Twamsifu Mwana, aliyetufia, Aliyetwaa dhambi akazifuta. 4. Twamsifu Mungu wa neema yote, Ametukomboa akatuongoza. 5. Tuamshe tena, tujazena pendo, Na moyoni uwashe moto wa Roho.

Mwokozi Umeokoa

Image
  1. Mwokozi umeokoa, Nimekuwa wako wewe. Damu imenisafisha; Sifa kwa mwana Kondoo.  Utukufu, Halleluya!  Sifa kwa Mwana Kondoo!  Damu imenisafisha,  Utukufu kwa Yesu! 2. Nilijitahidi sana Ila sikupata raha; Bali kwa kumtegemea Nilipata Baraka. 3. Daima namwegemea Damu ikifanya kazi, Nikioga kwa chemichemi Itokayo Mwokozi. 4. Sasa nimewekwa wakfu; Nitaishi kwako wewe: Fahari nashuhudia Ya wokovu wa bure. 5. Nasimama kwake Yesu, Ameponya roho yangu; Ameniondoa dhambi, Anifanye mzima. 6. Nilikuwa kifungoni, Niliteswa na dhambi, Nilifungwa minyororo Yesu akanifungua. 7. Sifa, ameninunua! Sifa, nguvu za wokovu! Sifa, Bwana huhifadhi! Sifa zake milele.